Showing posts with label SPORTS. Show all posts
Showing posts with label SPORTS. Show all posts

Thursday, August 28, 2014

Kikosi cha Timu ya Manchester United Ndicho Chenye Gharama Zaidi Kwenye Premier League kwa Sasa

Ghali: Kiasi cha £60m za Angel Di Maria kuja Manchester United toka Real Madrid imefanya jumla ya pesa za kusajili kikosi cha United kuwa zaidi ya £400m 
Kusajiliwa kwa Angel Di Maria wiki hii kumefanya jumla ya pesa zilizotumika kwa ajili ya kusajili wachezaji wa kikosi hicho kufika £401.2m - huku ikiaminika kiasi hicho cha pesa kinaweza kuongezeaka kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Tuesday, August 12, 2014

Picha ya Steven Gerrard Alipokuwa Akishangilia Liverpool Ilipofunga Goli Kwenye Mechi Dhidi ya Fulham Yashinda Tuzo ya Picha Bora Msimu Uliopita [PICHA]

Picha iliyopigwa na mpiga picha wa Sportsmail, Kevin Quigley, imeshinda tuzo ya picha bora ya Premier League kwa msimu uliopita, pale alipompiga nahodha wa Liverpool Steven Gerrard alipokuwa akishangilia mara baada ya kufunga kwenye mechi ya ugenini walipocheza na Fulham msimu uliopita.

Tuesday, June 10, 2014

Jennifer Lopez Kutoimba Kwenye Ufunguzi wa Kombe la Dunia

Mwanamuziki Jennifer Lopez hatoweza kuimba wimbo rasmi wa Kombe la Dunia kwenye sherehe za ufunguzi wa michuano hiyo nchini Brazil, Fifa imetangaza.

Monday, June 09, 2014

Filippo Inzaghi Achukua Nafasi ya Clarence Seedorf Kuifundisha AC Milan

Klabu ya AC Milan amemfukuza kazi kocha wake Clarence Seedorf baada ya kipindi kisichozidi miezi mitano toka ashike nafasi hiyo, huku ikimtaja Filippo Inzaghi kama mrithi wake.

Mchezaji huyo wa zamani wa Italia Inzaghi, 40, amesaini mkataba wa miaka miwili kuifundisha timu hiyo huku akiachana na kazi ya kufundisha timu ya vijana ya timu hiyo.

Tuesday, June 03, 2014

David Beckham Anafikiria Kurudi na Kuendelea Kucheza Soka

David Beckham amesema anafikiria kurudi na kuendelea kucheza soka. "Naanza kujifikiria binafsi je naweza kucheza tena? Hivi kweli naweza kurudi? Je nitaweza kutoka kwenye kustaafu na kuanza kucheza?'" alisema Beckham.

Monday, June 02, 2014

Etoo Ampa Kijembe Kingine Mourinho kwa Aina ya Mtindo ya Ushangiliaji wa Kibabu Kizee [PICHA]

Mchezaji huyo mwenye miaka 33 kwa mara nyingine tena ameonekana kumpa kijembe meneja wa timu ya Chelsea, Jose Mourinho, mara baada ya kufunga goli na kushangilia kwa mtindo wa kibabu kizee walipocheza dhidi ya Ujerumani siku ya Jumapili.

Thursday, May 29, 2014

Malcolm Glazer Aliyekuwa Mmiliki wa Manchester United Afariki Dunia

Aliyewahi kuwa mmiliki wa klabu ya Manchester United, Malcolm Glazer, amefariki dunia mnamo siku ya Jumatano akiwa na umri wa miaka 85.

Glazer, aliyeinunua  United mwaka 2005, pia anamiliki timu ya kwenye ligi ya NFL iiitwayo Tampa Bay Buccaneers, ambao ndio waliotangaza habari ya kifo chake kwenye mtandao wao.

Saturday, April 19, 2014

Yaya Toure: Asema Anastahili Kuheshimika Zaidi ya Anavyoheshimika Sasa

Mchezaji wa timu ya Manchester City na Ivory Coast kiungo Yaya Toure anaona ya kwamba haesabiki kama ni kiungo bora Duniani kwa sababu anatokea Africa.

Wednesday, April 16, 2014

Kutana na Mchezaji Mwenye Miaka 18, Mlinzi wa Chelsea Anayelipwa £20,000 kwa Wiki Ambaye Hajawahi Kucheza Kwenye Kikosi cha Kwanza cha Timu.. na Pia Hategemei Kucheza kwa Siku za Karibuni

Ndani ya Emirates hapo kesho Alhamisi jioni, mchezaji anayelipwa hela nyingi kwenye historia ya Kombe la FA kwa vijana anategemea kucheza kwenye timu yake ya Chelsea katika mchezo wa pili wa nusu fainali dhidi ya Arsenal.

Anaitwa Andreas Christensen, ambaye  hakuna mtu aliyewahi kumuona uwanjani, ametimiza umri wa miaka 18 mnamo April 10. Analipwa £20,000 kwa wiki huku akiwa hajawahi kucheza kwenye kikosi cha kwanza cha timu yake ya Chelsea.

Monday, April 14, 2014

Liverpool Kileleni Ikiifunga Man City 3-2

Wachezaji wa Liverpool wakishangilia mara baada ya Philippe Coutinh kuandika bao la tatu lililoipa timu yake bao la ushindi kwa jumla ya magoli 3-2.

Wednesday, April 09, 2014

HABARI YA KUSIKITISHA: Nguli wa Mchezo wa Mieleka wa WWE, Ultimate Warrior Afariki Dunia

Siku chache baada kutoka kwenye WWE Hall of Fame na miaka 18 kurudi kwenye shirikisho hilo, nguli wa mchezo wa mieleka, The Ultimate Warrior amefariki Dunia.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa WWE, nyota huyo wa mchezo wa mieleka amefariki akiwa na miaka 54.

Rekodi Mbovu ya Bayern Dhidi ya Timu za Uingereza Itatusaidia Kupata Ushindi - Asema Moyes

Pale unapokutana na mtihani mkubwa kwenye taaluma yao, ni vyema wakati mwengine kutumia njia ndogo mbadala.

Hapo jana usiku ndani ya Allianz Arena, David Moyes alialikwa kwenda kuangalia rekodi za hivi karibuni za Bayern Munich dhidi ya timu za Uingereza na kupata tumaini.

Chelsea Yaiua PSG Dakika za Majeruhi na Kutinga Nusu Fainali [PICHA]

Goli la dakika za majeruhi lililofungwa na Demba Ba limeiwezesha timu ya Chelsea kuingia kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya Klabu Bingwa Barani Ulaya mara baada ya kuifunga timu ya Paris St-Germain kwa wastani wa 3-3, huku timu ya Jose Mourinho ikifaidika na matokeo hayo kutokana na kuwa bao moja la ugenini walilolipata wiki moja iliyopita kwenye mechi ya kwanza iliyozikutanisha timu hizo jijini Paris, Ufaransa.

Tuesday, April 08, 2014

Howard Web Apigwa Chini Kuchezesha Pambano la Liverpool na Man City Huku Mark Clattenburg Akipewa Nafasi

Refa toka Uingereza atakayechezesha Kombe la Dunia Howard Webb, amepata pigo baada ya kuondoshwa kuchezesha mechi kati ya Liverpool na Manchester City.

Sunday, April 06, 2014

Brendan Rodgers Kutumia Uzoefu Wake Alipopanda Mlima Kilimanjaro Kuisaidia Liverpool Kutwaa Ubingwa

Brendan Rodgers anaamini bado hayupo tayari kusherehekea ubingwa wa Liverpool kwa kuweka bendera ya ushindi wa Ligi Kuu ya Uingereza katikati ya Anfield.

Jamaa huyu ambaye aliwahi kupanda mlima Kilimanjaro ameonya kwamba bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili Wekundu hao waweze kusherehekea ubngwa wa Ligi Kuu  kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 24.

Monday, March 24, 2014

Picha za Kwanza za Uwanja wa Beckham Unaotegemea Kujengwa Ndani ya Miami [PICHA]

Picha za kwanza za uwanja wa David Beckham unategemea kujengwa ndani ya Miami zimeonyeshwa kwenye MailOnline Sport.

uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 25,000 walioketi, unategemea kujengwa kwenye Ufukwe wa Miami, huku pia ukiwa na mgahawa na ukumbi wa disco.



Cheki picha zaidi hapo chini...

Friday, March 21, 2014

Ni Mpambano wa Daudi na Goliati - United Wapangwa na Bayern Robo Fainali Ligi ya Mabingwa

Timu ya David Moyes Manchester United wamepangwa kukutana na mabingwa watetezi Bayern Munich kwenye droo lililopangwa leo. Jose Mourinho na timu yake ya Chelsea akikutana uso kwa uso na Zlatan Ibrahimovic na timu yake ya PSG.

Yanga na Simba Zapigwa Faini Millioni 25 kwa Uharibifu wa Viti vya Uwanja wa Taifa

Klabu za Yanga na Simba zimeagizwa kulipa jumla ya sh. milioni 25 kutokana na uharibifu wa viti na vurugu zilizofanywa na washabiki wao kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na Al Ahly ya Misri iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Thursday, March 20, 2014

Mke Wangu Ana Shida Kuliko Shida Alizoazo Robben - Pe Guardiola

Kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola ametania kuwa huwa anapata wakati mgumu zaidi kufafanua juu ya mbinu yake ya kubadili wachezaji kwa mke wake Cristina kuliko anavyopata shida hiyo kumueleza mchezaji kama Arjen Robben.

Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona mara kadhaa amekuwa akiwapumzisha wachezaji wake wenye uwezo mkubwa akiwemo Mholanzi huyo kutokana na ukubwa wa kikosi cha timu aliyonayo.

Thursday, March 13, 2014

Rais wa Bayern Munich Jela Miaka Mitatu na Nusu kwa Kukwepa Kodi

Rais wa timu ya Bayern Munich Uli Hoeness amekutwa na hatia ya kosa la kukwepa kulipa kodi na Mahakama ya nchini Ujerumani siku ya Alhamisi na kuhukumiwa kwenda jela kwa miaka mitatu na nusu.

Wakili wa Hoeness baadae alitangaza kwamba wana mpango wa kukata rufaa kwenye Mahakama Kuu ya haki nchini Ujerumani.