Thursday, November 20, 2014

Video ya Wimbo Mpya Diamond Platnumz - Nitampata Wapi [TAZAMA]

Hiki hapa ni kichupa kipya cha msanii mahiri wa Bongo Fleva Diamond Platnumz. Kiaangalie kisha pale chini tiririka na mtazamo wako kwa vile ulivyokiona...!

Friday, September 26, 2014

Mwanaume Ajichubua Ngozi kwa Kutumia Acid Ili Afanane na Michael Jackson [PICHA]

Jamaa mmoja ambaye ni shabiki mkubwa wa Michael Jackson nchini Brazil ameamua kutumia acid ili kuingarisha ngozi yake ili aweze kufanana na nguli huyo wa muziki wa pop duniani.

Imeelezwa kwamba jamaa huyo hutumia kiasi cha £2,000 kununua vipodozi vya aina mbalimbali ali aweze kufanana na Michael.

Apple Yakiri KUPINDA kwa Simu Mpya ya iPhone 6 Ila Wamesema 'Ni kwa Nadra Sana' [PICHA]

  • Msemaji wa Apple ameeleza kwamba ni wateja wanane tu ndio ambao waliopeleka malalamiko ya kupinda kwa simu zao aina ya iPhone 6 Plus.
  • Kiwanda hicho kikubwa kimesema vitu vipya vilivyoingizwa kwenye simu hiyo mpya ni chuma kisichoshika kutu, sehemu ya kuingizia ya  titanium inserts na kioo kigumu kuwahi kutokea kwenye dunia ya utengenezwaji wa simu. 
Kampuni ya Apple Inc ilijikuta ikiingia kwenye hasara ya kujimudu mnamo siku ya Alhamisi, ikizungumzia kile kilichokuja kujulikana kama 'BendGate' kwa kusema kuwa malalamiko ya wateja juu ya tatizo hilo la iPhones ni machache sana tofauti na ukaribu wa ukweli wenyewe.

Friday, September 05, 2014

Huu Hapa ni Ujio Mpya wa Samsung na Kitu cha Galaxy Note Edge [PICHA]

Haya tena wale wapenzi wa teknolojia hasa gajeti, hapo jana Samsung walizindua flagship yao kutoka familia ya Galaxy note ambayo inakwenda kwa jina la Samsung Galaxy Note edge.

Simu hii ina kioo kilichojikunja tofauti na flat screen tulizozoea, kwa sasa hii ndio highest end phone kutoka Samsung.

Picha zaidi hapo chini..

Monday, September 01, 2014

Polisi Ujerumani Wamuokoa Diamond Kutoka kwa Mashabiki Wenye Hasira [PICHA]

Ukumbi uliharibiwa na washabiki mjini Stuttgart, Ujerumani
Usiku wa Jumamosi ya Tarehe  30, Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri, mwanamuziki nyota wa mziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul a.k.a Diamond Platnumz alijukuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart, Ujerumani, mara baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show yake.

Imeelezwa kwamba mashabiki hao waliokuwa wamelipa tiketi za kiasi cha Euro 25 kwa kiingilio ambapo walihadiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku, lakini walijukuta wakisubiri hadi majira ya saa10 usiku ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.

Thursday, August 28, 2014

Kikosi cha Timu ya Manchester United Ndicho Chenye Gharama Zaidi Kwenye Premier League kwa Sasa

Ghali: Kiasi cha £60m za Angel Di Maria kuja Manchester United toka Real Madrid imefanya jumla ya pesa za kusajili kikosi cha United kuwa zaidi ya £400m 
Kusajiliwa kwa Angel Di Maria wiki hii kumefanya jumla ya pesa zilizotumika kwa ajili ya kusajili wachezaji wa kikosi hicho kufika £401.2m - huku ikiaminika kiasi hicho cha pesa kinaweza kuongezeaka kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Tuesday, August 19, 2014

Nicki Minaj na Drake Kwenye Picha Matata za Video Yake Mpya ya Anaconda [PICHA]

Hakika Nicky yuko juu na ataendelea kuwa hivyo.... Utakapopata nafasi ya kuiona video ya wimbo wake mpya unategemea kutoka siku ya Jumatano, hakika utakubaliana nami.

Tuesday, August 12, 2014

Picha ya Steven Gerrard Alipokuwa Akishangilia Liverpool Ilipofunga Goli Kwenye Mechi Dhidi ya Fulham Yashinda Tuzo ya Picha Bora Msimu Uliopita [PICHA]

Picha iliyopigwa na mpiga picha wa Sportsmail, Kevin Quigley, imeshinda tuzo ya picha bora ya Premier League kwa msimu uliopita, pale alipompiga nahodha wa Liverpool Steven Gerrard alipokuwa akishangilia mara baada ya kufunga kwenye mechi ya ugenini walipocheza na Fulham msimu uliopita.

Wednesday, August 06, 2014

Hakika Beyonce Hatokuja Kuipenda Hii! Mwanamke Aweka Picha Mtandaoni Inayomuonyesha Mtoto Wake Anafanana na Jay Z [PICHA]

 Picha ya mtoto anyefanana na Jay Z imetapakaa kwenye mitandao kwa sasa, huku mashabiki wakitania juu ya rapa huyo huyo toka Brooklyn kuwa na mtoto wa siri.

Hakuna ushahidi wa zamani unaojitosheleza kuhusu picha hiyo, picha ambayo inamuonyesha mwanamke akiwa anacheka huku akiwa amewashika watoto wawili.

Sunday, June 15, 2014

Ungependa Kuwa Muwakilishi wa Tanzania Kwenye Shindano la Big Brother Mwaka Huu...? Hii Inakuhusu

Kampuni ya MultiChoice Africa inayoandaa mashindano ya Big Brother Africa imetangaza tarehe ya usaili wa shindano hilo mwaka huu katika nchi mbalimbali za Afrika.

Waandaaji hao wameitaja nchi ya Rwanda mwaka huu kuwa miongoni mwa nchi zitakazokuwa na washiriki katika shindano hilo mwaka huu ambapo mshindi ataondoka na kibunda cha $300,00.

Tuesday, June 10, 2014

Jennifer Lopez Kutoimba Kwenye Ufunguzi wa Kombe la Dunia

Mwanamuziki Jennifer Lopez hatoweza kuimba wimbo rasmi wa Kombe la Dunia kwenye sherehe za ufunguzi wa michuano hiyo nchini Brazil, Fifa imetangaza.

Monday, June 09, 2014

Filippo Inzaghi Achukua Nafasi ya Clarence Seedorf Kuifundisha AC Milan

Klabu ya AC Milan amemfukuza kazi kocha wake Clarence Seedorf baada ya kipindi kisichozidi miezi mitano toka ashike nafasi hiyo, huku ikimtaja Filippo Inzaghi kama mrithi wake.

Mchezaji huyo wa zamani wa Italia Inzaghi, 40, amesaini mkataba wa miaka miwili kuifundisha timu hiyo huku akiachana na kazi ya kufundisha timu ya vijana ya timu hiyo.

Happy Birthday: The Kokomaster D'Banj Atimiza Miaka 34 Leo

Mkali toka Naija, Dbanj leo ameongeza mwaka mwengine kwenye maisha yake. Hongera kwake na wote waliozaliwa siku na tarehe kama hii akiwemo Chris Wamarya...!

Kim Kardashian Asema Kanye West Ameyabadili Maisha Yake [Ujumbe wa Birthday]

Mnamo siku ya Jumapili Kanye alitimiza miaka 37, mke wake Kim Kardashian alitumia mtandao wa kijamii kusherehekea naye huku akiweka wazi kwa kuandika ujumbe kwamba "Kanye ameyabadilisha maisha yake kwa njia nyingi. Haishangazi kuona havai kihivyo." lol!

Sunday, June 08, 2014

Msichana wa Bongo Movie Aliyedaiwa Kula Uroda na Mbunge Akana Kuwa Sio Yeye Kwenye Picha Hizo



Picha chafu zinazodaiwa kuwa za star wa filamu nchini Shamsa Ford na mbunge wa Chadema, Salvatory Machemli, zimeanza kusambaa kwa kasi mitandaoni tangu jana.

Picha hizo zinawaonyesha wawili hao wakiwa kitandani kwenye mahaba mazito, hata hivyo picha hizo zinaonekana kutia shaka kuwa sio halisi ni za kutengenezwa ingawa hatuna uhakika kwa asilimia zote kwasababu msichana anayedaiwa kuwa Shamsa Ford ana umbo tofauti na la star huyo.

Diamond Ashindwa Kupata Tuzo za MTV Base

Msanii aliyekuwa akiiwakilisha Bongo kwenye tuzo za MTV Base, Diamond Platnumz ameshindwa kutwaa tuzo mara baada ya tuzo alizokuwa akigombania kuchukuliwa na wanamuziki toka nchi nyingine.
Tuzo ya Best Collaboration ilichukuliwa na Uhuru na wimbo wake uitwao Tjukutcha ambayo amemshirikisha Professor Oskido & Dj Bucks huku tuzo Best Male ikienda kwa Davido kutoka nchini Nigeria.

Kauli ya Kwanza ya Diamond Mara Baada ya Tuzo za MTV Base

Mara baada ya kumalizika kwa tuzo za Mtv Base huku mwanamuziki aliyewakilisha Bongo Diamond Platnumz kushindwa kupata tuzo, kupitia ukurasa wake wa Facebook msanii huyo aliandika hili kama kauli yake ya kwanza.

Mzee Small Afariki Dunia

Muigizaji mkongwe nchini Said Ngamba maarufu kama Mzee Small amefariki dunia siku ya Jumamosi majira ya saa 4 usiku akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar.

Thursday, June 05, 2014

Kutaka Kuwa na Makalio Makubwa Kumemponza Dada Huyu, Hebu Mcheki Alivyoharibika

Kwa wale wadada wanaotumia dawa za uongeza makalio yao wakiamini kuwa ndio wataonekana wazuri na kuwavutia wanaume, au haujatumia ila unafikiria kutumia siku moja,angalia hapa alafu utapata jibu utumie au ubaki na maumbile yako ya halisi

Chanzo: Hotnewzdaily

Ndoa ya Flora Mbasha Yalala Chali, Flora Adaiwa Kuhamia kwa Gwajima

Flora Mbasha akiwa na mumewe Emmanuel Mbasha.
BAADA ya kudumu kwa zaidi ya miaka 10, imebainika kuwa ndoa ya mwanamuziki mahiri wa muziki wa Injili Bongo, Flora na mumewe Emmanuel Mbasha ipo chali kwa maana ya kuanguka huku ikidaiwa kuwa, kusimama imara tena inawezekana lakini ni kazi kubwa, Amani limefukunyua mazito.
Hilo limejitokeza wiki moja baada ya madai ya mwanaume huyo kudaiwa kumbaka shemeji yake na kesi ipo polisi.

Wednesday, June 04, 2014

Je ni Kweli Kwamba Beyonce Ana Mahusiano ya Siri na Mlinzi Wake [PICHA]

Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni, inasemekana kwamba Jay Z anapatwa sana na wivu kutokana na ukaribu wa Beyonce na mlinzi wake aitwaye Julius (mtalaka mwenye mtoto mmoja), akidhani kuwa wawili hao wana mahusiano.

Huyu ndiye yule yule mlinzi aliyejaribu kumlinda Jay Z dhidi ya shambilizi la kwenye lifti. Jamaa yupo karibu sana na Beyonce, mara zote mikono yake huwa ipo karibu ya mwanamuziki huyo.