Wednesday, October 23, 2013

Hii ni Shule ya Kwanza Duniani Inayotoa Mafunzo ya Ngono, Ada Yake ni £1,400 Kwa Temu (MUHIMU ISOME)

Hii ni shule ya kwanza inayotambulika rasmi Duniani kwa kutoa mafunzo ya ngono, ikifunza aina za mitindo ya kufanya ngono na namna ya kumuhudumia mwenza kwa mbinu mbalimbali.

Kwenye kila darasa katika kila shule mara zote hutokea kuwepo kwa mtoto ambaye huwa hafanya homework zake. Ndio maana ake, mpaka ilipokuja kutokea kufunguliwa kwa milango ya chuo hicho kilichopo Austria kwenye jiji la Vienna kinachojulikana kwa jina la Austrian International Séx School.

Shule hiyo hutoza £1,400 kwa temu moja, huku kikitoa mafunzo hayo kwa njia ya nadhalia na vitendo.

Wanafunzi wa shule hiyo huchanganywa na kuishi kwenye hostel moja ambapo hushauliwa wasaidiane kufanya ‘assignments’ zao.

Mkuu wa shule hiyo - Ylva-Maria Thompson - mtu ambaye huwezi mshangaa, ni nyota ya filamu za ngono na ni mtangazaji wa vipindi vya ngono kwenye TV.

Mwanamke huyo mwenye miaka 51 amesema: ‘Nia ni kuwafanya watu wawe wapenzi wazuri, kufahamu aina mbalimbali za mitindo ya kufanya ngono, namna ya kumshughulikia mwenza wako, kuzifahamu sehemu nyeti za mwili na kuwafundisha watu namna nzuri za ushiriki wa tendo la ngono.

Licha ya hivyo shule hiyo imekuwa ikipata vikwazo kadhaa, ambapo matangazo ya TV yanayoonyesha watu wakifanya ngono yamepigwa marufuku, huku wengi wakisema shule hiyo ipo kwa ajili ya kufanya biashara ya ngono.

Kuna yeyote anayependa kwenda kusoma shule hii japo kwa mwaka mmoja...?

1 comment: