Thursday, January 16, 2014

Hawa ni Makahaba Waliwafanya Marapa Mashuhuri Kuzama Kwenye Penzi Zito - Amber Rose, Blac Chyna, Maliah Michel [PICHA]

Yalipita ni zile siku ambazo ili mwanamke aweze kupata mwanaume ilibidi awe mwanamke bora kweli kweli.

Siku hizi wanaume wengi weusi hupenda kuwa na wanawake ambao kwa namna moja ama nyingine mwanzoni walionekana kuwa wameshindikana nao huchukua jukumu la kuwabadilisha kuwa mademu wa ukweli.

Kanye West kwa Amber ni mfano tosha kuwa mmoja kati ya wanaume waliowapenda wasichana walioshindikana kuwafanya wawe wanawake haswa.

Wiz Kalifa alizama kwenye mapenzi kwa Amber Rose naye aliweza kumbadilisha kuwa mwanamke anayeheshimika na jamii.

Rappa Tyga alizama kwenye mapenzi na kahaba maarufu aliyejulikana kama Black Chyna, hii ni mara baada ya kumuona akiwa anafanya kazi yake kwenye klabu moja ya usiku, kwa sasa wamechumbiana na wana mtoto mmoja.

Mfano mwengine ni kama ilivyo kwa Amber ambaye amebadilika na kuwa mwanamke anayejiheshimu tofauti na mwanzoni, kama unakumbuka aliwahi kuwa na mahusiano na Kim na Kanye.

Hii ni kuthibitisha kwamba hata wale wasichana ambao tunaona kwamba wameshindikana kabisa kwenye jamii yetu inabidi tujue kwamba nao wanaweza kubadilika na kupenda kweli.

Ishu kuu hapa ni juu ya hawa marapa au wanaume kuzama kwenye mapenzi na hawa wanawake, kuna mifano mingi ningeweza kukuwekea ila kwa hiki nnachotaka kukifikisha hapa hii michache inatosha.

Nimekuwa nikijiuliza nyota au maceleb wa kibongo kama wanaweza kufunguka na kuwa wazi juu ya kutoka na makahaba, binafsi na labda wengi wetu tunajua kwamba huwa wanakutana nao japo wengi wao hufanya kwa siri.

Je mwanaume wa Kitanzania anaweza kufunguka ya kuwa anatoka na kahaba mpaka ifike hatua ya kumuoa?

Inawezekana kwa sasa mahusiano yanayojilikana sana kumuhisisha kahaba na mwanamuziki ni kati ya Wiz na Amber, naamini hii inatokana na ukweli kuwa wanaendana.

Ikumbukwe mwanzoni Wiz alikuwa anatoka na Natalie Nunn ambaye alionekana kwenye video chafu ya Olu Mantain na katika mchakato wa video hiyo ndipo alipokutana na Amber Rose na ikawa hivyo.
Kanye alianza, alionyesha Ulimwengu kwamba mtu yeyote anweza kuwa na mahusiano ya kawaida hata akiwa na tofauti gani na ndipo mahusiano yake na Amber Rose yalipoanza.


Tyga, Black Chyna na Mtoto wao

Black Chyna
Siku hizi Black Chyna anavaa vitu vya thamani vinavyotengenezwa na wanamitindo wakubwa yote ni kwa hisani ya mpenzi wake Tyga.

Black Chyna
Labda nikukumbushe kitu kingine ambacho inawezekana ulikuwa hukifahamu, achana na Rihanna, mnamo mwaka 2009 kipindi ambacho Drake alikuwa anatoka kwenye game, alikutana na kahaba aitwaye Maliah Michel na kuzama naye kwenye dimbi la mapenzi kiasi cha kufikia hatua Drake alindika wimbo kumzungumzia msichana huyo.

Licha ya mapenzi yake kwa Riri, bado Drake alikuwa anaenda kupitia mlango wa nyuma kwa kahaba huyo, inasemekena kwamba nyimbo nyingi za Drake zinazozungumzia kuumizwa kimapenzi zimekuwa zikimlenga msichana huyo.

Drake na Maliah Michel
Kwa kumalizia tu, kama ulikuwa hufahamu, mwanamuziki Eve E na Lady Gaga kabla hawajawa wenye majina waliyonayo nao sasa pia nao walianzia kwenye makahaba.

Eve E

No comments:

Post a Comment