Friday, December 06, 2013

Mandela Afariki Dunia


KWA UFUPI:

Mandela amekuwa akisumbuliwa na
maradhi kwenye mapafu kwa muda
mrefu, alilazwa na baadaye
kuruhusiwa kutoka hospitali ambapo
mauti  yamemkuta akiwa nyumbani 
kwake mjini Pretoria.

RAIS wa kwanza wa Afrika Kusini na mpinga siasa za ubaguzi wa rangi, Nelson Mandela amefariki nchini humo akiwa na umri wa miaka 95.
Taarifa za kifo chake zimetangazwa na rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma ambaye amesema Mandela amefariki majira ya saa 2.50 usiku wa Alhamisi kwa saa za Afrika Kusini.

Mandela amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwenye mapafu kwa muda mrefu, alilazwa na baadaye kuruhusiwa kutoka hospitali ambapo mauti yamemkuta akiwa nyumbani kwake mjini Pretoria.

Tayari viongozi mbalimbali duaniani wameshaanza kutuma salamu za rambirambi kwa familia na taifa la Afrika Kusini.

Viongozi hao ni pamoja na Rais Barack Obama wa Marekani na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-Moon.


CHANZO: Gazeti Mwananchi

No comments:

Post a Comment