Wednesday, December 18, 2013

Kutana na Mtoto wa Miujiza Aliyezaliwa Tarehe 11.12.13 Mida ya Saa 14:15 [PICHA]


Mara nyingi mtoto wa kwanza wa mama yeyote huwa ni wa matukio na mambo mengi sana anapozaliwa - ila siku ambayo mtoto wa Chelsea Johnson alizaliwa ilifanya kuwa na kitu kikubwa cha ziada kukikumbuka na kwa sababu maalum kabisa.

Sio tu kwamba alikuwa kama Landon-Jonah Johnson ambaye alizaliwa mnamo December 11, 2013, ila pia alifanya timing ya ajabu kwa kuingia Duniani, hii ni baada ya mtoto huyo kuziliwa mnamo majira ya saa 14:15 hivyo kufanya siku na muda aliozaliwa kusomeka hivi 11/12/13 14:15.

Chelsea, mwenye miaka 21, kutoka Rawmarsh, Rotherham, alisema kwamba mtoto wake ni wa ‘miujiza’.

“Ni mtoto maalumu,” alisema. “Nasubiri kwa hamu kuja kumueleza kipindi atakapokuwa mkubwa, na kwamba anatambua ni aina gani ya tukio lilikuwa
.” 

No comments:

Post a Comment