Thursday, November 21, 2013

Kiwanja cha Vágina: Kinatengenezwa Nchini Qatar kwa Ajili Kombe la Dunia - Muonekano Wake Wafananishwa na Sehemu za Siri za Mwanamke [PICHA]


Muundo wa kiwanja cha kwanza kati ya viwanja vipya vitakavyojengwa kwa ajili ya mashindano ya kombe la Dunia nchini Qatar mwaka 2022 umetolewa.... na mfano wake kimuonekano unaonekana kufanana na sehemu za siri za mwanamke (cheki picha hapo juu).

Huu ni moja kati viwanja vitakavyotengenezwa vikiwa na full AC ukiwa na uwezo wa kuchukua watu 40,000 utakaoitwa Al-Wakrah Stadium ambao unategemea kukamilika mnamo mwaka 2018.
Wachoraji wa ramani za majengo wameonekana kukwazwa na ana aina hii ya mchoro wakisema una muonekano wa kama sehemu za siri za mwanamke. Ila wenyewe wamekanusha na kusema mchoro wa kiwanja hicho kitakachotumia mamilioni ya dolla umetokana na aina ya boti za kizamani maarufu kama ngalawa ambazo kiasili zilikuwa zinatumika na wavuvi wa nchi ya Qatar.

Chanzo: LIB

1 comment:

  1. UJENZI WA UWANJA UNAKIUKA SANA HAKI ZA BINADAMU

    Fuata link kwa maelezo zaidi
    http://www.policymic.com/articles/74231/qatar-s-vagina-stadium-distracts-from-heinous-human-rights-abuses

    ReplyDelete