Thursday, May 02, 2013

Baba Wa Chris Brown, Sitaki Mwanangu Atoke na Rihanna

Chris Na Riri
Baba wa mwanamuziki maarufu wa RnB Chris Brown, ana mawazo sawa na kama ambavyo Wamarekani wengi huutokea kusma pale limapokuja suala la yeye kutoka na Rihanna.... anafikiri haikuwa sahihi kwa wao kurudiana tena.

Kwenye mahojiano na gazeti la NY Daily News, Clinton Brown alisemakwamba, japo kuwa anaelewa vile ambavyo mwanae anavutiwa na RiRi, ila ni bora kila mmoja akawa kivyake: alilieleza gazeti hilo:

“Binafsi hakika sikupenda yeye na Rihanna warudiane.”

Clinton Brown amabye alitengana na mama yake wa mwanae wakati Chris akiwa na miaka sita, anasema haoni sababu ni kwa nini uhusiano huo unaokuja na kwenda uendelee, ikiwa uhusiano wenyewe hauna muendelezo mzuri.

No comments:

Post a Comment