Wednesday, April 24, 2013

Kutana Na Samsung Galaxy S4

Binafsi nimebahatika kuziona aina nyingi ya simu za Android, huku teknolojia hiyo ikizalisha aina nyingi za simu na kila kukicha zikiwa zinaboreshwa kuwa zenye nguvu zaidi kwa kipindi cha miaka kadhaa sasa.
Google na makampuni ya utengenezaji wa simu hizo wamekuwa wakizipa vitu vingi vya ziada. Ila sasa naamini umefika muda ambapo kile kidogo ndio kinakuwa na mambo mengi zaidi.
Nahofia tumefika wakati huo, kwa maana simu mpya ya Samsung Galaxy S4 ni simu moja kali sana kuanzia muundo wake na hadi matumizi yake. Ikiwa na upana wa Ichi 5, kioo chake kikiwa kidogo kimeongezeka upana, ukilinganisha na Galaxy S III.Japo S4 yenyewe ina ng’aa zaidi na ni ndogo kwa wastani. Huku kioo chake kikiwa kina akisi zaidi, kikiwa na inch 441 pixels ukilinganisha na 272 za S III. S4 ina kioo kizuri na cha kukufanya uipende zaidi.

No comments:

Post a Comment