Saturday, April 20, 2013

D'banj : Sijampata Mwanamke Sahihi

Hii inashangaza….. kwa sababu kwenye mahojiano yake aliyoyafanya na Toolz kwenye Tv ya Ndani, D'banj alisema  kwamba yeye ni mtu mwenye furaha kwa sababu anatoka na mwanamke ambaye yupo nae kwa muda sasa.
Jana wakati anafanyiwa mahojiano na Seun Apara wa Thisday, D'banj alisema kwamba yeye yupo singo na hajampata mwanamke sahihi mpaka sasa.
D'banj alimueleza Seun:
"Nimekuwa kwenye mahusiano na wanawake wengi ila nisingependa kuongea kuhusu wao, sababu wengi kati yao wameenda na mambo yao au wameolewa. Sina ninachijutia kabisa sababu mimi bado ni kijana na sijaoa, japo mama yangu anataka nitulie. Mama yangu ananipenda na binafsi namfanya aelewe kwamba sio kama sitaki kuoa, ila bado sijampata mwanamke sahihi. Kama ataweza kunitafutia mwanamke sahihi , anaweza kuniita.

No comments:

Post a Comment