Tuesday, December 10, 2013

Toilet Paper Zenye Picha ya Rais Obama Zauzwa kwa $4.99 kwa Rola Ndani ya Marekani


Maduka kwenye majimbo ya Kusini nchini Marekani yamejiingiza kwenye kimbembe kutokana na kuuza toilet paper zimechapwa picha ya Rais wa nchi hiyo Barack Obama.

Mtandao wa Houmatoday.com, ambao unajihusisha na habari za mji wa Louisiana, hivi karibuni ulitoa habari juu ya tukio hilo ambapo wakazi wa eneo hilo waliziona tishu hizo zikiuzwa kwenye duka jirani na kwao.



Mwanamke aliyeitwa Linda Williams, alighafirika alipoyaona mabunda ya tishu hizo alipokuwa akiingia kwenye duka hilo. Aliueleza mtandao wa wa Houmatoday.com, “Kwa muda wa miaka 52 nilioishi, sijawahi kuona picha ya Rais kwenye mabunda ya toilet paper.”

Meneja wa duka linalouza toilet paper hizo alisema makaratasi hayo ni moja kati ya bidhaa inayonunuliwa sana. Alieleza Houmatoday.com, “Hatujaribu kuikataza kwa mtu yeyote, ila ni swala tu la kibiashara.”

No comments:

Post a Comment