Monday, December 09, 2013

Kanye West: 'Mimi Ndiye Mandela Ninayefata’


Kanye West kwa mara nyingine tena anashambuliwa, hii ni mara baada ya hivi karibuni kusema kwamba muda si mrefu atakuwa ni mtu mkubwa kama nembo ya mtetea haki za binadamu zaidi ya Nelson Mandela.

Kwenye mahojiano aliyoyoyafanya na WGCI radio ndani ya Chicago, rapa huyo wa Kimarekani alisema kwamba kifo cha kiongozi huyo aliyefariki akiwa na miaka 95 hatimaye kitawafanya watu wamuangalie zaidi yeye Kanye West kwa mafaniko yake.



Kanye alipoulizwa, kwa mtazamo wake, kwamba anaweza kumrithi Mandela kama kiongozi, alijibu,

“Mimi ndiyo Mandela ninayefata. Nina miaka 36, na nikiangalia kwenye kila kitu ambacho nimefanikiwa, ni swala tu la kulinganisha ndilo litakaloleta maana. Mpaka nakuja fika miaka 95, nitakuja kuwa ni shujaa mkubwa kuliko alivyowahi kuwa."

No comments:

Post a Comment