Sunday, November 03, 2013

Jifunze Namna ya Kuweka na Kutumia BBM Kwenye Kompyuta au Laptop Yako


Kwa namna moja ama nyingine nina hakika hii inaweza ibadilisha siku yako, unajua nini nini? Sasa unaweza ku-PING ukiwa na Kompyuta au Laptop yako. Ni rahisi sana, mara baada ya kufuata hatua zifuatazo utakuwa na uwezo kuweka BBM kwenye Kompyuta yako kuweza ku-PING na watu wote ulionao kwenye BBM.

Mahitaji ya Msingi kufanikisha hili.....

1. Fanya ku-Download Android SDK, unaweza ku-download HAPA
2. Baada a ku-download, extract hilo bando la Android SDK kwenye Kompyuta yako.
3. Kisha download file la BBM apk HAPA

Nawezaje kuweka BBM kwenye Kompyuta yangu 
1. Nenda kwenye folda la kifurushi ulichoki-extract cha adt.
2. Fungua SDK Manager.exe

3.Kwenye window ya sdk-manager chagua Tools - Manange avds
4. Kisha Create a new Android Virtual Device hakikisha RAM ya komputa yako ni kubwa zaidi ya 512 MB na kisha anzisha Virtual Device ambayo utakuwa umeitengeneza.


Sasa inakiri (copy) file la BBM.apk uliloli-download kwenye hili folda uliloli-extract: /sdk/platform-tools/ kiasi kwamba hilo folda linatakiwa liwe :/sdk/platform-tools/BBM.apk

Kisha lisogeze folda /sdk/platform-tools/ ukitumia file explorer. Chagua File-Open Command Prompt ndani ya msingi wa tools folder.

Ingiza maneno haya (adb install BBM.apk) bila kuweka braketi, subiri kwa dakika kadhaa kwa BBM kuweza kuwa imeingia kwenye Virtual Device yako.

Fungua BBM app kutoka kwenye App launcher, na faurahia kuwa ku-PING kwa kutumia Kompyuta yako. Naamini utaipenda.... Tafadhali washirikishe na wenzako waweze kuijua na kufurahia huduma hii kwa kubofya HAPA

1 comment: