Wednesday, July 31, 2013

Nashindwa Kujizuia Kutofanya Mapenzi na Wateja Je Nifanyeje..? (BARUA)


Nimekuwa nikifanya mapenzi na wanaume ninao wahudumia kwenye baa moja ambapo huwa nafanya kazi na hakika nimekuwa nikijirahisisha na kutumika kiurahisi.

Ni mwanamke ambaye nipo singo na nina umri wa miaka 28. Nimekuwa nikifanya kazi ya kuuza vinywaji laini na vigumu na kwenye moja ya baa iliyopo kwenye vituo vikubwa kwa muda wa miaka mitatu sasa. Wengi kati ya wateja wetu ni madereva wa maroli, wengi wao hutokea kuvutiwa na mimi ambapo huishiakuniachia hela kama keep change. Huwa nawapa namba yangu ya simu na kuonana nao mara baada ya kazi.

Ngono ni kitu kitamu na chenye hisia za ajabu kwa maana wakati mwengine hujikuta asubuhi nikiwa nipo ndani ya roli au nikiwa na mwanaume kitandani, mtu ambaye wakati mwengine sikumbuki hata tulikuatana vipi na kuahidiana nini hasa.

Wiki iliyopita kulikuwa na mtu ambaye nilimpenda, tulifanya mapenzi matamu. Muda tu baada ya kuingia ndani tulivuana nguo na kuanza kulana denda kwa sana, alikuwa ni mstaarabu na nilivutiwa naye.

Baada ya muda tukavaa nguo bila kuongea neno lolote. Alipokuwa anaelekea mlangoni alisema "ntakutafuta". Nilijua hakuwa mkweli juu ya kuniona tena. Kwa maana ndivyo ambavyo wanaume wengi wamekuwa wakiniambia ila kiukweli huyu alikuwa tofauti.

Ila nashindwa kujizuia kuacha kulala na wanaume ambao nilishawahi kukutana nao. Wakati mwengine najisikia kama kuonyesha kuwa kweli namaanisha juu ya nnachokisema ila bado naishia kujiona mimi ni mrahisi na niliyetumika sana. Kiukweli nahitaji kuacha hili.

Nahitaji kupata mtu ambaye nitatulia naye na kuanzisha familia ila siwezi kusema hapana kwenye ngono, japokuwa wakati mwengine huwa napendelea tu ku-kiss na kushikana ila huishia pale pale, Sijui huwa nafanya nini hasa yaani ni kama sijielewi.

Kwa nini siwezi kuwa na mwanaume kwa zaidi ya usiku mmoja.....?

No comments:

Post a Comment