Saturday, April 27, 2013

Gabrielle: Naonekana Kijana Sababu Natoka Na Vijana

Gabrielle Union
Muigizaji toka Hollywood mwenye umri wa miaka 40, Gabrielle Union amehusishwa kwenye orodha ya wanawake 100 wa kipekee duniani na jarida la People Magazine.

Si kitu cha kushangaza kwamba Gabrielle Union alichaguliwa kuwa mmoja kati ya wanawake wazuri kwa mwaka huu.
 Ameungana na viwango vya kina Halle Berry, Kelly Rowland na Kerry Washington kwenye toleo hilo linalowahusu nyota wakali toka Hollywood.
 Alipoulzwa amewezaje kujiweka na kuonekana bado kijana na mrembo, alijibu:
"Nilianza kunywa galoni la maji kwa siku nilipokuwa katikati ya miaka ya thelathini. Yamebadilisha kila kitu kutoka kwenye kuujenga uzito, nywele, ngozi, kucha na mfumo wa usagaji wa chakula. Na kwa kuongeza, naonekana kijana sababu natoka na vijana. Naamini hiyo ndio sababu na inafanya kazi vizuri kwangu.

Amelieleza jarida hilo kwamba katika umri wa miaka 40, ndio muda ambao siku zote alikuwa anataka kuwa.
Kwa sasa Gabrielle anatoka na nyota wa mpira wa kikapu nchini Marekani aitwae, Dwayne Wade, ambae amemzidi miaka 9.

No comments:

Post a Comment