Saturday, May 25, 2013

Naomi Cambell: Ana Miaka 43 Na Bado Ana Miguu Mizuri Kwenye Tasnia Ya Wanamitindo

Naomi Cambell
Mwanamitindo maarufu Duniani Naomi Campbell hakika bado yupo juu ya mchezo. Baada ya miaka karibia 30 kuwa mmoja kati ya wanamitindo walio juu zaidi, mwanamitindo huyo mkubwa aliyezaliwa ndani ya jiji la London akianzisha maonyesho mbalimbali kwa sasa bado anaonekana hana dalili ya kushuka chini.
 
Naomi bado anatembea juu ya majukwaa, akishiriki kwenye kampeni kubwa za fasheni, akipozi kwa nguo fupi na hivi karibuni akiishiriki kama muandaaji wa vipindi vya TV kitu ambacho kinazidi kuing'arisha nyota yake.
 
Japokuwa njiani kumekuwa na nyakati tofauti za kupanda na kushuka, nyota huyo ameweza kufanikiwa kuyapita mengi na kusonga mbele.
 
Akiwa kama alama ya mitindo leo hii anatimiza miaka 43, inawezekana akawa hayupo pale alipokuwa mwaka jana (ndani ya Israel na aliyekuwa boyfriend wake wa Kirussia billionea Vladislav Doronin) na anaweza kuwa sio mwanamitindo maarufu na mwenye nguvu kuliko wote Duniani (hongera kwa Giselle). Ila unajua ni nini...? Naomi bado ni makali na pia ana miguu mizuri kwenye tasnia.

No comments:

Post a Comment