Tuesday, April 16, 2013

RICK ROSS AMBA RADHI KWA KUHALALISHA UBAKAJI

Rapa na bosi wa Maybach Music Rick Ross hatimae ameomba radhi kutokana na mashairi ya wimbo wake wa U.O.E.N.O ambao unachochea na kuhalalisha ubakaji. Rappa huyo ameomba radhi kupitia akaunti yake ya Twitter akiandika ‘I don’t condone rapè. Apologies for the #lyric interpreted as rapè. #BOSS’. Kuomba kwake radhi kumekuja siku moja baada ya kikundi kimoja cha wanawake kuandamana mpaka kwenye ofisi ya Reebok jijini New York. Reebok ni moja kati ya wadau wa Rick Ross. Baadhi ya mashairi kwenye wimbo huo uitwao U.O.E.N.O yanasema ‘Put molly all in her champagne, she ain’t even know it/I took her home and I enjoyed that, she ain’t even know it’.

No comments:

Post a Comment