Tuesday, April 16, 2013

AKACHA UALIMU KUJIKITA KWENYE UMALAYA

Chris Rock alishawahi kusema jukumu la msingi la baba ni kuhakikisha anamlea mtoto wake kiukamilifu, ila Emma Nicholson, 36, amepingana na hilo. Mwanamke huyo toka shule ya msingi iliyopo Hull nchini Uingereza, wiki nane zilizopita aliamua kuachana na kazi hiyo na kuamua na kujikita na shughuli za uchezaji mziki wa kwenye majukwaa (Stripper). “Unapowashawishi vijana wadogo, ni hatari sababu wakati mwengine mnakuwa ni watu wa aina moja," Nicholson alisema, kwa mujibu wa gazeti la Sun. “Watu wapo tofauti na si vyema kuwahukumu.” Nicholson, ambae alianza kucheza mziki miaka saba iliyopita, kwa sasa ameanzisha studio yake ambapo huwafundisha wasichana wengine utamu wa kazi hiyo. "Nilipoanza tu nilifahamu kwamba nahitaji mlingoti wangu hata nikiwa nyumbani," Nicholson alisema, kwa mujibu wa gazeti la Metro. "Mimi na marafiki zangu hutumia mda mwingi wa usiku tukinywa chupa za waini kisha huenda kwenye mlingoti wangu." MLINGOTI: Kama umeshawahi ona baadha ya filamu, kuna wale wasichana kwenye klabu za usiku (Casino) huwa wanazunguka kwenye milingoti.

No comments:

Post a Comment